Skip to main content

MHITIMU WA DARASA LA SABA ABAKWA,AUAWA KISHA KUTUPWA MAKABURINI


Mwili wa mtoto Lucia Thomas ambaye amefanyiwa ukatili ukiwa ndani ya Jeneza ukiagwa na kusafirishwa kwenda wilayani Bunda mkoani Mara kwa ajili ya mazishi.
Baadhi ya majirani,ndugu,jamaa na marafiki wakiwa nje kwa ajili ya kuaga mwili wa marehemu.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Mkoani, Salvatory Edward akisisitiza kufungwa kwa vituo bubu vya kufundishia wanafunzi kwenye mtaa ambao anauongoza. 
Mchungaji wa Kanisa la Heri wenye moyo safi , Samwel Samson akihubiri na kutoa neno la faraja kwa familia.
Baadhi ya wananchi wakiwa kwenye hali ya masikitiko na maombolezo. Picha na Joel Maduka,Geita

***
Mtoto Lucia Thomas mwenye umri wa miaka 12 amekutwa akiwa ameuawa na mwili wake kutupwa eneo la makaburi mtaa wa mkoani mjini Geita.
Mwenyekiti wa mtaa wa Mkoani, Salvatory Edward amedai pamoja na kunyongwa hadi kufa, mwili wa mtoto huyo aliyehitimu darasa la saba mwaka huu katika Shule ya Msingi Kiandege wilayani Bunda pia ulikuwa na dalili za kubakwa kabla ya kuuawa.
Mama mkubwa wa mtoto huyo Bi, Grace Thomas amesema hata wao wameshangazwa na tukio hilo kwani mtoto huyo alikuja Geita akitokea Jijini Mwanza akiwa salama na kwamba kwa mtu ambaye ametenda ukatili huo ni vyema kwa vyombo vya sheria vikafuatilia kwa umakini hili waweze kumchukulia hatua za kisheria.
Mama Mzazi wa Mtoto huyo Bi, Mary Thomas alisema mwanaye alitoka nyumbani juzi Alhamis saa 12:30 jioni akiwa ameongozana na mtu aliyesema ni mwalimu wake wa masomo ya maandalizi ya kujiunga na kidato cha kwanza kwa maelezo kuwa anaenda kuchukua karatasi za mitihani ya somo la Uraia.
Aidha ameongeza kuwa baada ya kuona usiku umeingia bila mtoto kurejea nyumbani, alikwenda kwa mwalimu mwingine aliyemtaja kwa jina moja la ambapo waliongoza hadi nyumbani kwa mwalimu aliyeondoka na mwanaye na kumkuta lakini akawatoroka kwa kujifanya anampa mtu begi alilolishika mkononi.
Baada ya mwalimu huyo kutorejea huku mtoto haonekani, waliendelea kumtafuta mtoto wake usiku kucha bila mafanikio ndipo alipoenda kutoa taarifa polisi alikotakiwa kurejea iwapo itapita saa 24 bila mtoto kurejea nyumbani.
“Kabla ya saa 24 kumalizika, taarifa zilinifikia kuwa mwili wa mwanangu umeonekana makaburini akiwa tayari amefariki huku ukiwa na michubuko shingoni na akiwa amefungwa kamba miguuni huku hana nguo ya ndani,” alisema Bi,Mary .
Kutokana na tukio hilo, uongozi wa serikali ya mtaa wa mkoani umepiga marufuku vituo vyote vya masomo ya ziada eneo hilo na kuwataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao kwenye shule zinazotambulika kisheria badala ya vituo vya vichochoroni.
Imeandikwa na Joel Maduka,Geita

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Tanzania yakiri ununuzi wa Bombadier uko matatani

Tindu Lissu Serikali ya Tanzania imekiri kudaiwa na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd kama ambavyo kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Tindu Lissu alivyo tangaza hivi karibuni. Kiongozi huyo amesema kuwa kumekuwa na athari za Serikali kuvunja mikataba ya wawekezaji wa nje kwani wanasheria wanaoishauri serikali wamekuwa hawatekelezi wajibu wao inawezekana ni kwa sababu ya kuogopa kutumbuliwa. Lissu ambaye ni mwanasheria Mkuu wa Chadema alidai Ijumaa kuwa utekelezaji wa ununuzi wa ndege ya tatu kutoka kampuni ya Bombadier ya nchini Canada umezuiliwa nchini Canada na kampuni hiyo ya ujenzi kwa kuwa inaidai serikali Dola 38.7 milioni za Marekani (Sh 87 bilioni). Vyanzo vya habari vinasema kuwa kampuni hiyo ilipewa kibali cha kukamata mali za Tanzania na Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro katika nchi za Ufaransa, Uholanzi, Uingereza, Ubelgiji, Uganda na Canada. Lakini kwa upande wake serikali imesisitiza kuwa licha ya deni hilo, ndege hiyo ita...