Skip to main content

Breaking News: Rais Magufuli Atangaza Baraza Jipya la Mawaziri


Rais John Magufuli ametangaza baraza jipya la mawaziri lililoongezeka kutoka wizara 19 hadi 21.


Wizara hizo zimeongezeka kutokana na wizara mbili kugawanywa huku nafasi za manaibu wapya zikiwa tano.

Akitangaza leo Jumamosi baraza hili jipya, Rais Magufuli amesema Wizara ya Nishati na Madini imegawanywa mara mbili, sasa kutakuwa na Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini.

Amesema hatua hiyo inatokana na umuhimu wa rasilimali hiyo kwa taifa na kwamba wizara hizo zote kila moja itakuwa na waziri na naibu wake.

Rais Magufuli ametaja mabadiliko mengine katika Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambayo kwa sasa kutakuwa na Wizara ya Kilimo inayojitegemea na nyingine itakuwa ni Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Amesema sababu za kufanya mabadiliko hayo ni kutokana na umuhimu wa sekta hiyo inayoajiri asilimia 75 ya Watanzania nchini hivyo ni vyema ijitegemee. Kila wizara itakuwa na waziri na naibu wake.

Mabadiliko mengine ni katika wizara ya Tamisemi baada ya kuweka nafasi mbili za manaibu waziri kwa sababu ni wizara inayogusa sehemu kubwa ya wananchi.

Pia yamefanyika katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Angalia orodha ya mawaziri hao hapa

1.Wizara ya Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora.

Waziri – George Huruma Mkuchik

2.Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Raisi, Muungano na Mazingira

Waziri – January Makamba

Naibu Waziri - Kangi Lugola

3.Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi Vijana, Ajira na Walemavu

Waziri – Jenista Mhagama

Naibu Waziri – Anthony Peter Mavunde

Naibu Waziri Walemavu – Stela Alex Likupa

4.Wizara ya Kilimo

Waziri - Charles John Tizeba

Naibu Waziri - Mary Mwanjelwa

5.Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Waziri - Makame Mbarawa

Naibu Waziri - Atashasta Nditiye

Naibu Wziri - Elias John Kwandikwa

6.Wizara ya Fedha na Mipango

Waziri - Dr Philip Mpango

Naibu Waziri - Dr Ashatu Kijaji

7.Wizara ya Nishati

Waziri - Medrad Matogoro Kalemani

Naibu Waziri - Subira Hamisi Mgalu

8. Wizara ya Madini

Wairi - Angela Kairuki

Naibu Waziri - Haroon Nyongo

9. Wizara ya Katiba na Sheria

Waziri – Palamagamba Kabudi

10. Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afika Mashariki, Kikanda na Kimataifa.

Waziri - Agustino Mahiga

Naibu Waziri - Dkt Susan Kolimba

11 .Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Waziri - Dr Hussein Mwinyi

12. Wizara ya Mambo ya Ndani

Waziri – Mwigulu Nchemba

Naibu Waziri - Hamad Masauni

13. Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Waziri - William Lukuvi

Naibu Waziri - Angelina Mabula

14. Wizara ya Maliasili na Utalii

Waziri – Hamisi Kigwangala

Naibu Waziri - Ngailonga Josephat

15. Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Waziri - Charles Mwijage

Naibu Waziri - Stella Manyanya

16. Wizara ya Elimu, Sayansi Teknolojia na Ufundi

Waziri - Joyce Ndalichako

Naibu Waziri - William Ole Nasha

17 .Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Waziri – Ummy Mwalimu

Naibu Waziri – Faustine Ndugulile

18. Wizara ya Habari, Utamadu, Wasanii na Michezo

Waziri - Dr . Harrison Mwakyembe

Naibu Waziri - Juliana Shonza

19. Wizara ya Maji na Umwagiliaji

Waziri - Isack Kamwelwe

Naibu Waziri - .Juma Hamidu Aweso

20. Mifugo na Uvuvi

Waziri - Luhaga Mpina

Naibu Waziri - Abdallah Ulega

21. Wizara ya TAMISEMI

Waziri – Suleiman Japho

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...