Skip to main content

VIDEO: Msigwa, Lema watema cheche Nairobi wakihojiwa kuhusu Tundu Lissu

Wabunge wawili wa Chadema wametumia mahojiano nje ya nchi kuzungumzia matatizo ya Tanzania wakisema hayawezi kumalizwa na mtu mmoja bali kwa mifumo imara ya mihimili ya Mahakama, Bunge na Serikali.

Wakizungumza katika mahojiano na Kituo cha Televisheni cha KTN cha Nairobi, Kenya  jana Jumapili walisisitiza umuhimu wa kuwa na Katiba Mpya ili kuipa nguvu mihimili hiyo.

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema ufisadi ambao Rais John Magufuli anaushughulikia sasa ulifanywa na watendaji waliokuwa chini ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Alisema chama hicho kimeongoza nchi tangu Tanzania ilipopata Uhuru, hivyo ufisadi huo ulifanywa na viongozi waliokuwa chini ya chama hicho.

“Ili tuwe na mfumo wenye nguvu tunatakiwa kubadilisha Katiba ili tuwe na Mahakama na Bunge huru,” alisema.

Lema alisema kumtegemea mtu mmoja hakuwezi kuleta mafanikio kama ambayo yamefikiwa na Kenya.

Alisema Katiba ikibadilishwa na kuwa na vipengele mbalimbali, vikiwemo vya kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na kumshtaki Rais akitoka madarakani Tanzania itakuwa imepiga hatua.

Alisema mabadiliko ya Katiba nchini Kenya si tu yataisaidia katika siasa bali katika kukuza uchumi wao.

“Uamuzi wa Mahakama ya Juu ya Kenya kufuta matokeo ya Rais si tu yatawasaidia kisiasa bali yatajenga imani hata kwa wawekezaji,” alisema.

Alisema wawekezaji wataongezeka nchini Kenya kwa sababu wanakuwa na imani na Mahakama.

Kwa upande wake, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa alisema Rais ana nguvu kuliko mihimili mingine na amekuwa akitoa maelekezo kwa mihimili hiyo.

“Bunge la Tanzania limetekwa na Serikali, wenzetu CCM wako wengi kuliko sisi wapinzani, wakikaa kwenye Party Caucus (vikao vya chama) yao wanaamua mambo yenye manufaa kwa chama chao,” alisema.

Alisema madhara ya wabunge wa CCM kufanya uamuzi wenye manufaa kwa chama hayawaathiri wapinzani tu, bali Watanzania kwa jumla.

Wabunge hao wako jijini Nairobi kumjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyelazwa katika Hospitali ya Nairobi baada ya kupigwa risasi Septemba 7 mwaka huu akiwa nyumbani kwake Area D, mjini Dodoma.

==>Wasikilize hapo chini
 

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...