Skip to main content

Polisi Dsm anayejiita 'Faru John' atakiwa kuhojiwa

Image result for polisi kanda maalum dar


Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amemuagiza Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Temeke kuhakikisha askari anayejiita Faru John anafikishwa ofisi kwake kuhojiwa akituhumiwa kwa rushwa.

Agizo hilo amelitoa leo Jumapili baada ya wakazi wa Mbagala kumlalamikia wakidai askari huyo amekuwa akiwakamata wafanyabiashara na kudai kwa nguvu rushwa ya Sh20,000.

Wananchi  hao wamelalamika kuwa, mfanyabiashara ambaye hatoi fedha hizo hufungwa pingu na kuzungushwa usiku kucha akiwa kwenye gari la polisi.

Kamanda Mambosasa aliyekuwa akisikiliza kero za wananchi wa Mbagala Zakhem amesema Jeshi la Polisi haliwezi kuwa na askari anayejipa jina la mzaha, huku akiwakandamiza wananchi.

Amesema huo ni mmomonyoko wa maadili kwa askari ambao kazi yao ni kulinda raia na mali zao, hivyo atawachukulia hatua wote watakaobainika kuomba na kupokea rushwa.

"Ninawaomba askari kuwalinda wafanyabiashara wenye mitaji midogo kama vile wakaanga chipsi. Kuwadai Sh20,000 eti kwa sababu wamechelewa kufunga biashara hilo sikubaliani nalo hata kidogo, lazima niwachukulie hatua," amesema Kamanda Mambosasa.

Pia, amekemea askari wanaodai rushwa kwenye vituo vya polisi ambavyo amesema vipo kwa ajili ya kutoa huduma.

Amewaagiza wakuu wa vituo kuhakikisha watu hawakai muda mrefu vituoni kwa kuwa kufanya hivyo ni kutengeneza mazingira ya kupokea rushwa.

Mkazi wa Mbagala, Thabiti Mohamed alisema kuna askari anayejulikana kwa jina la Faru John amekuwa akiwakamata wafanyabiashara, wakiwemo wauza chipsi ambao huchelewa kufunga maduka hadi saa tano usiku na huzunguka nao usiku kucha wakiwa wamewafunga pingu.

Mohamed alisema askari hao huomba kwanza Sh20,000 ili kuwaachia na wasipozitoa ndipo hufungwa pingu na kupakiwa kwenye gari.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Kibangulile, Mashaka Selemani amemuomba Kamanda Mambosasa kuwahamisha askari wa Kituo cha Polisi Maturubai akisema hawakamati wahalifu bali wapo kwa ajili ya kupokea rushwa.

"Askari hawa kazi yao wanapomkamata mtuhumiwa wanampeleka ofisi ya Serikali ya Mtaa Mikwambe, wanapofika kazi yao wanataka fedha kwa nguvu. Wasipopata wanawapiga na kuwabambikia kesi. Tumefuatilia wanakusanya hadi Sh1 milioni kwa siku, hivyo wameshazoeleka tunataka waondolewe Mbagala," alisema Selemani

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...