Skip to main content

Lori lapata ajali na kuua mmoja na kujeruhi

Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina moja la William amefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa vibaya baada ya lori walilokuwa wakisafiria kupasuka gurudumu la mbele upande wa kushoto na kuacha njia eneo la gogoni Kibamba Manispaa ya Ubungo.

Ispector wa Polisi wa kituo cha Kimara, Seni Magembe amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema imetokea majira ya saa 3 asubuhi huku majeruhi wa ajali hiyo akiwepo dereva wa lori hilo Shabani Ramadhani (29) amelazwa katika hospitali ya Tumbi pamoja na mwili mwili wa marehemu Wiliam ambaye alikuwa utingo wa lori lenye namba za usajili T. 955 ACP aina ya Volvo likiwa na tela lake lenye namba T 724 AAN umehifadhiwa katika hospitali hiyo hiyo ya Tumbi.

Mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo Abuu Ramadhani mkazi wa Gogoni amesema walisikia kishindo kikubwa majira ya saa 3 asubuhi na walipofika eneo hilo maarufu kama Gogoni kwa bi Mtumwa walikuta gari hilo likiwa tayari limepinduka.

Ajali hiyo imetokea wakati jeshi la polisi mkoani Pwani , kitengo cha Usalama barabarani likiendelea na operesheni maalumu ya ukaguzi wa makosa mbalimbali ya barabarani kwa  madereva wa malori  sambamba na kuwapima kiwango cha ulevi .

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...