Skip to main content

Kijo-Bisimba atoa neno kuhusu wasiojulikana

Watetezi wa haki za binadamu kwa umoja wao wametaka watu wasiojulikana waweze kuchukuliwa hatua za kiusalama mara moja ili kubaini wahalifu hao wanajihusisha na vitendo vya kikatili dhidi ya watu mbalimbali nakuzuia hali hiyo isiendelee kutokea tena.

Akizungumza leo Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Sheria na Haki za binadamu, Dkt Helen Kijo-Bisimba amesema kwamba matukio hayo kukomeshwa kutajenga amani na umoja kwa watu.

Kama hatua za kisheria na za kiusalama hazitachukuliwa kwa tukio hili la kinyama litaleta shida kwa taswira ya nchi ya Tanzania kwenye nchi zingine na kuchafua serikali. Kwani hakuna nchi duniani iliyoingia katika kadhia hizi ni zikabaki salama" Bi Kijo-Bisimba
Pamoja na hayo watetezi hao  wamemuunga mkono Rais kutokubali kunyonga baadhi ya wafungwa ambao wamehukumiwa kifo

Mbali na hayo Kituo hicho kimewataka viongozi wa dini kuchukua hatua madhubuti kukemea kwa nguvu kubwa matukio hayo kwani mwisho wa matukio haya ni kuvunjika kwa amani ya nchi. Pia amewataka viongozi  wa siasa kujadili masuala ya usalama na haswa suala la utekwaji na mashambulizi ya kinyama kwa wananchi na kutoa mapendekezo yatakayoleta suluhu ya kudumu kwa usalama wa nchi.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...