Skip to main content

Jiwe kubwa sana kupita karibu na dunia

Map showing path of Asteroid Florence

Jiwe kubwa zaidi kuwahi kupita karibu na dunia katika kipindi cha karibu karne moja linatarajiwa kupita karibu na sayari ya dunia umbali wa karibu maili milioni 4.4 , kimesema kituo cha masuala ya anga za juu cha Marekani, Nasa.
Vipimo vya Florence vilikadiria umbali wa maili 2.7 sawa na kipenyo cha 4.4 na kwamba jiwe hilo halina tisho kwa dunia kwa karne zijazo
Mawe mengine yaliyowahi kupita karibu na dunia, yalikadiriwa kuwa ni madogo sana.
Mawe hayo ambayo yana umbo la vifusi upande wa kushoto ni masalia yaliyobaki wakati wakuundwa kwa jua na sayari.
Jiwe la Florence - lililogundulika mnamo mwaka 1981- linaweza kuwa mara 18 ya wastani wa umbali baina ya dunia na mwezi.
"Florence ni jiwe kubwa zaidi kuwahi kupita karibu na dunia yetu tangu kuanzishwa kwa mpango wa shirika la anga za mbali la Marekani NASA wa kuchunguza na kubaini mawe yaliyopo karibu na dunia ," Amesema Paul Chodas, meneja wa kituo cha NASA kinachochunguza vitu vilivyopo karibu na dunia katika taarifa yake.
Ugunduzi wa mwaka 2017 ni wa jiwe la angani lililopo karibu tangu mwaka 1890 na ukaribu huo hautawahi kutokea hadi baada miaka 2500, shirika la masuala ya anga la Marekani limeongeza.
Mpango wa wanasayansi kuchunguza ukaribu wa jiwe, kwa kutumia mtambo wa rada wa ardhini unafanyika California na Puerto Rico.
Wataalam wa anga za juu pia watakuwa wakilichunguza jiwe hilo yamesema majarida ya masuala ya anga ya Sky na Telescope.
Jiwe ni rahisi kuliona kwa kutumia kifaa cha uchunguzi , si kwa sababu tu ni kubwa , lakini pia kwa sababu huakisi 20% ya mwanga wa jua ambao huchoma kwenye sehemu yake ya chini.
Kinyume chake mwezi huakisi wastani wa 12% pekee.
Kitu chenye ukubwa wa Florencekinaweza kuwa na athari ya kugonga dunia. Wanasayansi wanaamini kuwa sasa wamebaini zaidi ya 90% ya miamba ya aina hiyo ya kutisha inayopita angani karibu na sayari yetu.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Tanzania yakiri ununuzi wa Bombadier uko matatani

Tindu Lissu Serikali ya Tanzania imekiri kudaiwa na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd kama ambavyo kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Tindu Lissu alivyo tangaza hivi karibuni. Kiongozi huyo amesema kuwa kumekuwa na athari za Serikali kuvunja mikataba ya wawekezaji wa nje kwani wanasheria wanaoishauri serikali wamekuwa hawatekelezi wajibu wao inawezekana ni kwa sababu ya kuogopa kutumbuliwa. Lissu ambaye ni mwanasheria Mkuu wa Chadema alidai Ijumaa kuwa utekelezaji wa ununuzi wa ndege ya tatu kutoka kampuni ya Bombadier ya nchini Canada umezuiliwa nchini Canada na kampuni hiyo ya ujenzi kwa kuwa inaidai serikali Dola 38.7 milioni za Marekani (Sh 87 bilioni). Vyanzo vya habari vinasema kuwa kampuni hiyo ilipewa kibali cha kukamata mali za Tanzania na Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro katika nchi za Ufaransa, Uholanzi, Uingereza, Ubelgiji, Uganda na Canada. Lakini kwa upande wake serikali imesisitiza kuwa licha ya deni hilo, ndege hiyo ita...