Skip to main content

AUAWA KWA KUCHOMWA KISU BAADA YA KUKUTWA NA MKE WA MTU CHUMBANI SINGIDA


Mtu mmoja anayejulikana kwa jina la Idd Selemani, (40), Mkazi wa Jineri katika Manispaa ya Singida ameuwa kwa kuchomwa na kisu sehemu mbalimbali za mwili wake na Mtuhumiwa aitwaye Khalid Rajabu, (45), fundi viatu na Mkazi wa Jineri baada ya mtuhumiwa huyo kumkuta akiwa na mke wake chumbani kwake.


Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida SSP Isaya Mbughi amesema tukio hilo  limetokea jana majira ya saa majira ya saa 9:30 alasiri.


Ameeleza kuwa  mbinu aliyoitumia mtuhumiwa kufanya tukio hilo kuwa ni kumvizia marehemu akiwa na mke wa mtuhumiwa aitwaye Mariam Ibrahimu, (25) mkazi wa Jineri wakiwa chumbani kwa mtuhumiwa ambapo mtuhumiwa huyo aliingia chumbani kwake kisha kufunga mlango na kuanza kumshambulia Marehemu na kumsababishia majeraha kisha kufariki muda mfupi wakati akipelekwa Hospitali ya Mkoa Singida.


Amesema chanzo cha mauaji hayo kuwa ni wivu wa kimapenzi.

 Jeshi la Polisi linawashikilia watuhumiwa Khalid Rajabu na mke wake kwa mahojiano na baada ya mahojiano kukamilika watuhumiwa watafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Kaimu Kamanda ametoa wito kwa Wananchi wote kwa kuwataka kuacha kujichukulia sheria mkononi bali watoe taarifa vituo vya Polisi pindi wanapopata migogoro yenye utata ili kuchukua hatua za kisheria na kuongeza kuwa wazazi/wanandoa wanatakiwa kuwa waaminifu katika ndoa zao ili kuepusha migogoro inayoweza kuleta athari.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...