Skip to main content

WATOTO WATATU WA LUCKY VICENT WALIOWASILI LEO WAWALIZA WATANZANIA WALIOENDA KUWAPOKEA UWANJA WA NDEGE WA KIA


SeeBait
Wazazi, watoto na watu mbali mbali wameshindwa kujizuia na kumwaga chozi walipokuwa wakiwapokea watoto Sadia Ismail, Doreen Eribariki na Wilson Tarimo, ambao wamerejea rasmi nchini wakitokea nchini Marekani walikokuwa wakipatiwa matibabu.

Watoto hao ambao ni manusura wa ajali iliyoua takriban wanafunzi 32 wa shule ya msingi Lucky Vicent, wamepokelewa na viongozi mbali mbali wa serikali wakiwemo Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Bi. Anna Mghwira, Mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu, wazazi na wanafunzi wa shule ya Lucky Vicent, waliwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Watu mbali mbali walihudhuria uwanjani hapo wakiwa na mashada ya maua kuwalaki huku kukiwa na burudani mbali mbali kutoka kwa sanii Mercy Masika wa Kenya, Angel Bernad wa Tanzania na Kwaya ya Shangwe kutoka jijini Arusha.

Shirika la Samaritan Purse la Marekani lilijitolea kusaidia watoto hao kuanzia usafiri na gharama za matibabu kwa muda wote ambao walikuwa nchini humo wakitibiwa, katika Hospitali ya Sioux City tangu mwezi Mei 15, kufuatia majeraha makubwa kwenye ajali kubwa waliyoipata tarehe 6 Mei 2017, wakitokea hospitali ya Mt. Meru Arusha.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...