Skip to main content

Ufafanuzi wa Taarifa za kuwepo tozo za ukiukwaji ukomo wa mwendokasi barabaran

Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa zinazozua mkanganyiko kwenye mitandao ya kijamii kuhusu faini zinazotoshwa na Wakala wa Usimamizi wa Barabara Tanzania (TANROADS) kwa madereva wanaozidisha mwendo wa magari au kufanya makosa mengine ya barabarani.

Kufuatia mkanganyiko huo, Balozi wa Usalama Barabarani (RSA) ambao hujitolea kutoa elimu ya usalama barabarani kuhakikisha watumiaji wote wa barabara wanakuwa salama.

Katika ufafanuzi huo uliotolewa na RSA, kwanza walianza kujibu swali ambalo liliulizwa na wengi kama TANROADS ina mamlaka ya kupiga faini kwa kosa la mwendokasi.

TANROADS kama mamlaka ya usimamizi wa barabara chini ya Sheria ya Barabara (ROADS ACT 2007) inayo mamlaka ya kuwaadhibu wale wote wanaokiuka mwendo uliooneshwa kwenye alama za barabarani au kadiri ya maelekezo yao.

Mamlaka haya wanayapata kwa mujibu wa kifungu cha 32(2) cha Sheria ya Barabara, Na.13 ya mwaka 2007. Hata hivyo, ili mtu atozwe faini chini ya sheria hiyo ni hadi atiwe hatiani.

Inayotia mtu hatiani ni mahakama, hivyo ukikamatwa na TANROADS unatakiwa kufikishwa mahakamani na huko ukipatikana na hatia uweze kutozwa kiasi cha shilingi 200,000 au jela mwaka 1, na sio vinginevyo.

Jambo jingine lilitotolewa ufafanuzi baada ya kuzua maswali ni kama kweli faini za barabarani zinazotozwa kwa kosa la mwendokasi sasa ni sh 200,000 na inagawanyika mara tatu yaani kiasi cha shilingi 90,000 kinaenda SUMATRA, Shilingi 30,000 kinaenda Polisi na inayobaki ni ya TANROADS.

RSA wameeleza kwamba, madai hayo ni upotoshaji. Faini ya chini ya sheria ya barabara ni shilingi 200,000 kwa kuzidisha mwendo kinyume na kifungu cha 32(2) na haigawanyiki.

“Haiwezekani kutozwa faini zaidi ya moja kwa kosa hilo hilo. Kwani sheria inasema mtu hataadhibiwa mara mbili kwa kosa hilo hilo alilolitenda mara moja. Iwapo mtu ameadhibiwa mara mbili adhabu hiyo ya pili ni batili. Ndio kusema kwamba, hata mamlaka zote 3 ziwepo pamoja, ukikamatwa umezidisha mwendo utaadhibiwa mara moja tu na mamlaka ile iliyokukamata.”

Mabalozi hao walilazimika kulielezea hilo baada ya kuwepo swali kama inawezekana mtu mmoja akaadhibiwa na mamlaka zote tatu kwa pamoja endapo zitakuwa barabarani kwa wakati mmoja eneo moja zinafanya operesheni.

Kuhusu uwepo wa sheria 3 kwa jambo hilo hilo moja la kuzidisha mwendo, imeelezwa kwamba kila sheria ilitungwa kipindi tofauti na nyingine na kila sheria inasimamiwa na mamlaka yake bila mamlaka moja kuiingilia nyingine.

SUMATRA anasimamia Transport licensing Act Cap 317 na kanuni zake, ambapo faini ni kati ya shilingi 200,000 na 500,000. TANROADS inasimamia Roads Act 2007 pamoja na kanuni zake za mwaka 2009, ambapo faini ni shilingi 200,000 huku Polisi wakisimamia Sheria ya Usalama Barabarani (Road Traffic Act Cap 168) ambapo faini yake ya papo kwa papo ni shilingi 30,000 bila kujali ukubwa au udogo wa kosa.

Kila mamlaka inasimamia sheria yake na kwamba mamlaka moja mfano Polisi hawawezi kukuandika faini kwa kutumia sheria ya TANROADS. Kama watataka kufanya hivyo watalazimika kukukabidhi kwa mamlaka hiyo.

Washirikishe na wenzako waweze kupata elimu ya usalama barabarani.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...