Skip to main content

Tundu Lissu Amlima Barua Jaji Mkuu.....Adai Wanasheria Waliosusia Mgomo Alioutangaza Hawana Mshikamano

Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), kimemwandikia barua Kaimu Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma, kumwelezea sababu za mgomo wao na jinsi wanasheria wanavyonyanyaswa na kuuawa.

Mgomo huo wa siku mbili unatokana na shambulio la mabomu katika Ofisi ya Mawakili ya IMMMA.

Barua hiyo ya TLS iliyotiwa saini na Rais Tundu Lissu, imesema mgomo wao wa siku mbili haumaanishi kupingana na Serikali au kuwaadhibu wateja ila kuhamasisha umma kuhusu mazingira ya hatari waliyopo wanasheria nchini.

Lissu alisema tukio hilo halikufanyika kwa bahati mbaya na matukio kama hayo ya kuwasumbua wanasheria wasifanye kazi zao ipasavyo, imekuwa sehemu ya maisha yao.

“Kwa mfano, Aprili 7, mwaka jana ofisi za Mwanasheria Said Omar Shaaban ambaye kwa sasa ni Rais wa Chama Wanasheria wa Zanzibar (ZLS), zilipigwa bomu na kuharibiwa, lakini hadi leo hakuna ripoti ya uchunguzi wa polisi.

“Wanasheria pia wamefungwa  kizuizini na wengine kukamatwa wakiwa mahakamani wakitekeleza majukumu yao ya kitaaluma na wengine wameuawa kikatili.

“Kwa mfano miaka michache iliyopita, wanasheria Profesa Jwani Mwaikusa na Dk. Sengondo Mvungi, waliuawa baada ya kuvamiwa na kupigwa na watu wasiojulikana.

“Machi mwaka juzi Wakili Philbert Gwagilo, alipotea katika mazingira ya kutatanisha na hakuna taarifa yoyote iliyotolewa kuhusu kupotea kwake,” alisema Lissu katika barua hiyo.

Akizungumzia kuhusu wanasheria ambao hawatagoma, alisema wanaotaka kwenda mahakamani waende kama wanaona wenzao kulipuliwa kwa mabomu ni sawa, ila wakae wakijua hawako salama.

“Tunataka tuhakikishiwe usalama wetu, siku mbili hizi tunataka wananchi nao wapaze sauti kuomba usalama wa wanasheria, au wanataka tufe wangapi ili wajue tunahitaji ulinzi?” alihoji Lissu.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Tanzania yakiri ununuzi wa Bombadier uko matatani

Tindu Lissu Serikali ya Tanzania imekiri kudaiwa na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd kama ambavyo kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Tindu Lissu alivyo tangaza hivi karibuni. Kiongozi huyo amesema kuwa kumekuwa na athari za Serikali kuvunja mikataba ya wawekezaji wa nje kwani wanasheria wanaoishauri serikali wamekuwa hawatekelezi wajibu wao inawezekana ni kwa sababu ya kuogopa kutumbuliwa. Lissu ambaye ni mwanasheria Mkuu wa Chadema alidai Ijumaa kuwa utekelezaji wa ununuzi wa ndege ya tatu kutoka kampuni ya Bombadier ya nchini Canada umezuiliwa nchini Canada na kampuni hiyo ya ujenzi kwa kuwa inaidai serikali Dola 38.7 milioni za Marekani (Sh 87 bilioni). Vyanzo vya habari vinasema kuwa kampuni hiyo ilipewa kibali cha kukamata mali za Tanzania na Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro katika nchi za Ufaransa, Uholanzi, Uingereza, Ubelgiji, Uganda na Canada. Lakini kwa upande wake serikali imesisitiza kuwa licha ya deni hilo, ndege hiyo ita...