Skip to main content

Tundu Lissu Amlima Barua Jaji Mkuu.....Adai Wanasheria Waliosusia Mgomo Alioutangaza Hawana Mshikamano

Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), kimemwandikia barua Kaimu Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma, kumwelezea sababu za mgomo wao na jinsi wanasheria wanavyonyanyaswa na kuuawa.

Mgomo huo wa siku mbili unatokana na shambulio la mabomu katika Ofisi ya Mawakili ya IMMMA.

Barua hiyo ya TLS iliyotiwa saini na Rais Tundu Lissu, imesema mgomo wao wa siku mbili haumaanishi kupingana na Serikali au kuwaadhibu wateja ila kuhamasisha umma kuhusu mazingira ya hatari waliyopo wanasheria nchini.

Lissu alisema tukio hilo halikufanyika kwa bahati mbaya na matukio kama hayo ya kuwasumbua wanasheria wasifanye kazi zao ipasavyo, imekuwa sehemu ya maisha yao.

“Kwa mfano, Aprili 7, mwaka jana ofisi za Mwanasheria Said Omar Shaaban ambaye kwa sasa ni Rais wa Chama Wanasheria wa Zanzibar (ZLS), zilipigwa bomu na kuharibiwa, lakini hadi leo hakuna ripoti ya uchunguzi wa polisi.

“Wanasheria pia wamefungwa  kizuizini na wengine kukamatwa wakiwa mahakamani wakitekeleza majukumu yao ya kitaaluma na wengine wameuawa kikatili.

“Kwa mfano miaka michache iliyopita, wanasheria Profesa Jwani Mwaikusa na Dk. Sengondo Mvungi, waliuawa baada ya kuvamiwa na kupigwa na watu wasiojulikana.

“Machi mwaka juzi Wakili Philbert Gwagilo, alipotea katika mazingira ya kutatanisha na hakuna taarifa yoyote iliyotolewa kuhusu kupotea kwake,” alisema Lissu katika barua hiyo.

Akizungumzia kuhusu wanasheria ambao hawatagoma, alisema wanaotaka kwenda mahakamani waende kama wanaona wenzao kulipuliwa kwa mabomu ni sawa, ila wakae wakijua hawako salama.

“Tunataka tuhakikishiwe usalama wetu, siku mbili hizi tunataka wananchi nao wapaze sauti kuomba usalama wa wanasheria, au wanataka tufe wangapi ili wajue tunahitaji ulinzi?” alihoji Lissu.

Comments

Popular posts

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Septemba 18

MAGAZETI YA LEO 2/10/2017