Skip to main content

TAARIFA KWA UMMA.


Image result for picha ya ndalichako

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inapenda kuutarifu umma kuwa taarifa zinazosambaa kwa kasi  kwenye mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari
“Serikali yapiga Marufuku Kusoma Degree bila kupita Kidato cha Sita,” tarifa hiyo siyo ya kweli na haijatolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mh. Joyce Ndalichako.
Wizara inapenda kuufahamisha umma kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako hajatangaza popote na kuwa taarifa hiyo haina ukweli wowote.
Profesa Ndalichako yuko Mkoani Kigoma kwenye ziara ya ufuatiliaji wa Miradi ya Elimu, inayotekelezwa kwa ushirikiano wa Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Wizara yake.
Vile vile Wizara inapenda kutoa wito kwa watanzania kuacha kutumia mitandao ya kijamii vibaya kwa kuupotosha umma kwa taarifa ambazo siyo sahihi na  hazina ukweli wowote.
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ina utaratibu wake wa kutoa taarifa hivyo inawaomba radhi wale wote waliopata usumbufu kutokana na kusambaa kwa taarifa hiyo.
Imetolewa na:
Mwasu Sware
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
19 Agosti, 2017

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...