Skip to main content

Shahidi Asimulia Alivyomsikia Tundu Lissu Akiikashifu Serikali

Shahidi  wa tano wa Jamhuri katika kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), amedai mahakamani kwamba alipomsikia mtuhumiwa akitamka Rais Dk. John Magufuli ni rais uchwara na ni rais dikteta, alisogea pembeni, hakuendelea kusikiliza.

Shahidi huyo, Timos Emekea (44), alidai hayo jana wakati akiongozwa kutoa ushahidi wake na Wakili wa Serikali, Paul Kadushi mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Mwambapa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Alidai aliona baadhi ya askari wanasogea kutokana na maneno ya Lissu na akahisi kuna kitu kinaweza kutoka, hivyo akajiondokea na safari zake.

Emekea ambaye ni mkazi wa Goba, alidai siku  hiyo ya tukio ya Juni 28, 2016 alikuwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akimdhamini mfanyakazi wake saa tano asubuhi.

Alidai akiwa mahakamani hapo, aliona umati wa wananchi, waandishi wa habari na Lissu ambaye huwa anamuona kwenye TV alizungumza maneno ambayo hakupendezwa nayo.

Wakili Peter Kibatala alimuhoji shahidi huyo kwamba Lissu aliyatamka maneno yaliyoandikwa kwenye hati ya mashtaka ama aliyoyaeleza katika ushahidi wake.

Shahidi alidai ni maneno yaliyoandikwa katika hati ya mashtaka na kwamba Serikali iliyotajwa ya kidikteta ni Serikali hii ya Tanzania.

Kibatala alipohoji ni wapi Serikali ya Tanzania imeandikwa kwenye hati ya mashtaka, alijibu hakuna.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 4, 2017.

Lissu ambaye pia ni Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Rais wa TLS na Mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anadaiwa kutoa kauli za uchochezi dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

Anadaiwa katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, alitoa kauli za uchochezi kuwa: “Mamlaka ya Serikali mbovu ni ya kidikteta uchwara, inahitaji kupingwa na kila Mtanzania kwa nguvu zote, huyu diktekta uchwara lazima apingwe kila sehemu. Kama uongozi utafanywa na utawala wa kijinga, nchi inaingia ndani ya giza nene.’’

Katika kesi hiyo, tayari mashahidi wawili wa upande wa mashtaka, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Kimweli na Staff Sajenti Ndege wamekwishatoa ushahidi wao.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...