Skip to main content

Sababu ya Moyo Kupanuka

Moyo kupanuka au kuwa mkubwa ni tatizo ambalo huathiri utendaji wa mfumo wa usambazaji damu mwilini.

Ni hali inayosababishwa na ukinzani wa moyo jinsi unavyotoa na kuingiza damu katika mishipa ya moyo na kuelekea sehemu mbalimbali za mwili.

Moyo kupanuka kutokana na kutokana na mazingira ya kusukuma damu kwa nguvu ya ziada tofauti na kawaida, hivyo kusababisha misuli ya moyo kuharibika. Wakati mwingine moyo hutanuka bila sababu zinazojulikana moja kwa moja. Pia, wakati mwingine moyo unaweza kutanuka kwa kipindi kifupi kutokana na mgandamizo kwenye mwili wako mfano ujauzito.

Hali nyingine ni tatizo la moyo ulilozaliwa nalo, kuharibika kwa moyo kutokana na mshtuko wa moyo, kudhoofu kwa misuli ya moyo au moyo kutodunda kwa mpangilio. Mazingira hayo huweza kusababisha moyo kutanuka.

Hali zingine za kiafya zinazohusiana na moyo kutanuka ni kama zifuatazo:

Kupanda kwa shinikizo la damu. Hali hii husababisha moyo kusukuma damu kwa nguvu zaidi ili kuifikisha sehemu mbalimbali za mwili. Hali inayosababisha misuli ya moyo kutanuka na kuwa minene hivyo kufanya moyo kuongezeka ukubwa.

Kupanda kwa shinikizo la damu kunaweza kusababisha ventrikali ya kushoto kupanuka na kufanya misuli ya moyo kudhoofika. Shinikizo la juu la damu pia hufanya sehemu ya juu ya moyo kutanuka.

Ugonjwa wa misuli ya moyo Ugonjwa huu husababisha misuli ya moyo kukakamaa na kusababisha moyo kujaribu kusukuma damu kwa nguvu zaidi kitu kinachoweza kusababisha moyo kutanuka.

Kupanda kwa shinikizo la damu kwenye mshipa wa damu unaounganisha moyo na mapafu Hali hii hujulikana kitaalamu kama Pulmonary Hypertension. Hii husababisha moyo kusukuma damu kwa taabu kwenda na kutoka kwenye mapafu ambako huwekewa hewa ya oksijeni.

Hali hii husababisha upande wa kulia wa moyo kutanuka au kuwa mkubwa.

Kuwapo maji kuzunguka moyo Maji kukusanyika kwenye mfuko unaobeba moyo, huweza kusababisha kuonekana mkubwa hasa baada ya kupiga picha ya x-ray.

Upungufu wa damu mwilini Kuwa na kiwango cha chini cha chembe hai nyekundu za damu hufanya ubebaji mdogo wa oksijeni kwenda sehemu mbalimbali za mwili, husababisha moyo kutumia nguvu nyingi kusukuma damu kwa haraka ili kuweza kusambaza oksijeni ndogo kwa haraka itosheleze mahitaji.

Kusukuma huko kwa haraka husababisha moyo kutanuka au kuwa mkubwa.

Matatizo ya tezi. Ikiwa tezi zinatoa homoni kwa kiwango kikubwa au kidogo, husababisha matatizo ya moyo yanayojumuisha utanuke na kuwa mkubwa.

Kuwapo kwa wingi wa madini chuma mwilini

Hali hutokea pale mwili unashindwa kutumia madini ya chuma vizuri. Hali hiyo husababisha madini haya kujijenga kwenye ogani mbalimbali za mwili, ikiwa ni pamoja na moyo.

Kuwapo kwa madini chuma kwenye moyo husababisha kutanuka kwa ventrikali ya kushoto na kuwa sababu ya kudhoofu kwa misuli ya moyo.

Magonjwa ya moyo kama Amyloidosis

Ugonjwa huu hutokana na protini isiyo ya kawaida inapozunguka kwenye damu. Protini hiyo ikifika kwenye moyo huweza kuziba baadhi ya mirija hivyo kuingilia utendaji wa kawaida wa moyo na kufanya moyo kutanuka.

Dalili za Moyo Kutanuka
Moyo kutanuka huonekana kwa picha ya X-ray ya kifua ingawa vipimo vingine vinahitajika ili kubaini ni nini kinasababisha moyo kutanuka.

Baadhi ya watu wenye moyo mkubwa hawana dalili za moja kwa moja, ingawa wengi hupata dalili kama kupumua kwa tabu, mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida, kujaa au kuvimba kwa mwili hasa miguu, wakati mwingine vidole kufa ganzi na kukakamaa.

Dalili nyingine ni kifua kubana au kuuma, kupata kizunguzungu, kuhisi hali ya mwili kunyong’onyea au kutokuwa na nguvu, kupoteza fahamu na kuzimia.

Moyo kutanuka ni hali ambayo inayoweza kutibiwa kwa urahisi ikiwa itagundulika mapema. Hivyo ni vyema kutafuta msaada wa kitabibu ikiwa unapata dalili za matatizo ya moyo.

Matibabu
Matibabu ya moyo mkubwa yanaweza kuhusisha matumizi ya dawa, kubadili mfumo wa maisha na wakati mwingine upasuaji. Mara nyingi moyo ukipanuka husababisha baadhi ya sehemu kwenye misuli ya moyo kutokufikiwa na damu, hivyo kusababisha tundu kwenye moyo au kidonda cha moyo na baadaye kupooza.

Kuepuka tatizo hili
Kuepuka ulaji wa nyama kwa wingi, hasa ile nyekundu, kupunguza matumizi makubwa mayai na maziwa kupindukia.

Punguza matumizi ya vyakula vya kusindikwa, epuka mafuta yatokanayo na wanyama, tumia yale yanayotokana na mimea kama alizeti, karanga, nazi na mawese, tena kwa kiasi kidogo.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Tanzania yakiri ununuzi wa Bombadier uko matatani

Tindu Lissu Serikali ya Tanzania imekiri kudaiwa na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd kama ambavyo kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Tindu Lissu alivyo tangaza hivi karibuni. Kiongozi huyo amesema kuwa kumekuwa na athari za Serikali kuvunja mikataba ya wawekezaji wa nje kwani wanasheria wanaoishauri serikali wamekuwa hawatekelezi wajibu wao inawezekana ni kwa sababu ya kuogopa kutumbuliwa. Lissu ambaye ni mwanasheria Mkuu wa Chadema alidai Ijumaa kuwa utekelezaji wa ununuzi wa ndege ya tatu kutoka kampuni ya Bombadier ya nchini Canada umezuiliwa nchini Canada na kampuni hiyo ya ujenzi kwa kuwa inaidai serikali Dola 38.7 milioni za Marekani (Sh 87 bilioni). Vyanzo vya habari vinasema kuwa kampuni hiyo ilipewa kibali cha kukamata mali za Tanzania na Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro katika nchi za Ufaransa, Uholanzi, Uingereza, Ubelgiji, Uganda na Canada. Lakini kwa upande wake serikali imesisitiza kuwa licha ya deni hilo, ndege hiyo ita...