Skip to main content

Rais Shein ameelezwa Vijana 55 wamekubali kuachana na Dawa kulevya

Zaidi ya vijana 50 wamekubali kuachana na utumiaji dawa za kulevya kufuatia ziara ya mkuu wa mkoa wa mjini magharibi katika maficho ya vijana hao huko kinazini ambapo mpaka sasa vijana hao wamepelekwa katika vituo vya kurekebisha tabia 'Sober House'.

Taarifa hiyo imetolewa na Ayoub mahmoud mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi mbele ya Rais ya wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein wakati akiwasilisha muhutasari wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika mkoa huo jana visiwani Zanzibar.

RC Ayoub amemueleza Rais Shein kuwa katika kuendeleza mapambano hayo mpaka sasa mashauri na kesi zimefikia 361 zinazowahusu watuhumiwa biashara za madawa ya kulevya na kwamba ziko katika hatua mbali mbali kwenye taratibu za kisheria.
Mkuu huyo wa mkoa yuko katika ziara ya siku tatu na Rais Shein ambayo imeanza jana katika Wilaya ya mjini na leo siku ya Ijumapili wataendelea na ziara katika wilaya ya Mjini magharibi 'A' na siku ya Ijumatatu atamalizia katika wilaya ya Magharibi 'B'

Ziara hiyo ni ya kwanza kwa Rais Shein tangu achaguliwe katika uchaguzi wa marudio mwaka jana, Na ni ya tatu tangu aingie madarakani mwaka 2010.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Tanzania yakiri ununuzi wa Bombadier uko matatani

Tindu Lissu Serikali ya Tanzania imekiri kudaiwa na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd kama ambavyo kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Tindu Lissu alivyo tangaza hivi karibuni. Kiongozi huyo amesema kuwa kumekuwa na athari za Serikali kuvunja mikataba ya wawekezaji wa nje kwani wanasheria wanaoishauri serikali wamekuwa hawatekelezi wajibu wao inawezekana ni kwa sababu ya kuogopa kutumbuliwa. Lissu ambaye ni mwanasheria Mkuu wa Chadema alidai Ijumaa kuwa utekelezaji wa ununuzi wa ndege ya tatu kutoka kampuni ya Bombadier ya nchini Canada umezuiliwa nchini Canada na kampuni hiyo ya ujenzi kwa kuwa inaidai serikali Dola 38.7 milioni za Marekani (Sh 87 bilioni). Vyanzo vya habari vinasema kuwa kampuni hiyo ilipewa kibali cha kukamata mali za Tanzania na Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro katika nchi za Ufaransa, Uholanzi, Uingereza, Ubelgiji, Uganda na Canada. Lakini kwa upande wake serikali imesisitiza kuwa licha ya deni hilo, ndege hiyo ita...