Skip to main content

Odinga kuwasilisha kesi kupinga ushindi wa Kenyatta leo

Odinga anadai mitambo ya tume ya uchaguzi ilidukuliwa kumfaa KenyattaOdinga anadai mitambo ya tume ya uchaguzi ilidukuliwa kumfaa Kenyatta


Muungano wa upinzani nchini Kenya National Super Alliance leo unatarajiwa kuwasilisha kesi ya kupinga ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 8 Agosti.
Mawakili wa muungano huo wanatarajiwa kuwasilisha kesi hiyo katika majengo ya Mahakama ya Juu mjini Nairobi.
Kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais yaliyotangazwa Ijumaa wiki iliyopita yanafaa kuwasilishwa kabla ya leo saa sita usiku, kabla ya kumalizika kwa siku saba tangu kutangazwa kwa matokeo.
Mgombea urais wa chama hicho waziri mkuu wa zamani Raila Odinga alikuwa ameapa kutopinga matokeo ya urais tena kortini kabla ya uchaguzi kufanyika na baada ya matokeo kutangazwa.
Lakini alibadilisha uamuzi huo na kutangazwa Jumatano wiki hii kwamba muungano wake ungefika kortini kupinga matokeo hayo.
Bw Odinga alisema ingawa muungano huo ulikuwa umeapa kutowasilisha kesi kortini wakati huu, waliona ni heri kufanya hivyo "kufichua uovu uliotokea wakati wa uchaguzi mkuu."
"Tumeamua kwenda kortini kufichua jinsi uongozi wa kompyuta ulivyofanikishwa...Hawa ni viongozi wa kompyuta. Kompyuta ndiyo iliwataga, kompyuta iliangulia, kompyuta iliwatoa. Vifaranga vya kompyuta."
Wafuasi wa upinzani wamekusanyika katika barabara za kuelekea majengo ya Mahakama ya JuuWafuasi wa upinzani wamekusanyika katika barabara za kuelekea majengo ya Mahakama ya Juu
Bw Odinga alisema mitambo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi IEBC ilidukuliwa na matokeo kuvurugwa kumfaa Bw Kenyatta ambapo kulikuwa na pengo kiasi fulani kati yake yeye na Bw Kenyatta muda wote wa kutangazwa kwa matokeo.
Aidha, kiongozi huyo aliishutumu tume ya uchaguzi akisema ilikuwa ikitangaza matokeo ya uchaguzi bila kutoa Fomu 34A za kuonyesha matokeo yalivyokuwa katika vituo vya kupigia kura.
Jamii ya kimataifa ilikuwa imehimiza upinzani, pamoja na wagombea wengine ambao hawakuwa wameridhishwa na uchaguzi, kutumia mifumo iliyowekwa kikatiba kutafuta haki.
Kwa mujibu wa matokeo ya IEBC, Rais Kenyatta alipata kura 8,203,290 huku naye Raila Odinga akipata kura 6,762,224.


Tarehe muhimu kesi ya kupinga uchaguzi wa rais

  • Agosti 18: Siku ya mwisho ya kuwasilsiha kesi
  • Agosti 20: Siku ya mwisho ya kuwasilisha nyaraka za kesi kwa wanaofaa kujibu kesi
  • Agosti 24: Siku ya mwisho kwa wanaofaa kujibu kesi kuwasilisha majibu
  • Septemba 1: Siku ya mwisho kwa Mahakama ya Juu kutoa uamuzi.
Uamuzi wa Mahakama ya Juu kuhusu kesi hiyo ni wa mwisho. kwa mujibu wa Katiba ya kenya, iwapo mahakama hiyo itaidhinisha ushindi wa Bw Kenyatta kiongozi huyo ataapishwa kuongoza kwa muhula mwingine tarehe 12 Septemba, siku saba baada ya kutolewa kwa uamuzi.
Iwapo mahakama hiyo itakubali malalamiko ya upinzani na kubatilisha ushindi wa Bw Kenyatta, basi uchaguzi mpya utafanyika katika kipindi cha siku 60 baada ya uamuzi kutolewa, kufikia tarehe 31 Oktoba.
Takwimu kutoka IEBC

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...