Skip to main content

Mwanamke Auawa Kikatili Ndani ya Pagala

Mwanamke mmoja amekutwa akiwa ameuawa na watu wasiyofahamika na mwili wake kutupwa kwenye nyumba ambayo haijamalizika kujengwa (Pagala) huku akiwa amefungwa kwenye mfuko wa sandarusi na kuzungushiwa nguo alizokuwa amevaa.

Hayo yamethibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoani Mwanza, DCP Ahmed Msangi na kusema tukio hilo limetokea tarehe 16.08.2017 majira ya saa 11:30 jioni katika mtaa wa Kitangiri kata ya Kitangiri Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.

DCP Msangi amesema mwili wa marehemu uliweza kuonekana mahali hapo baada ya watoto waliokuwa wakicheza eneo hilo kuona kifurushi kilichotupwa kwenye Pagala ndipo walipotoa taarifa kwa mama yao na baadaye kutoa taarifa kwa uongozi wa Mtaa pamoja na kituo cha Polisi.

Aidha, Kamanda Msangi amesema mwili wa marehemu haukuwa na jeraha lolote bali uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa wauaji walimuua kwa kumziba pumzi kisha kwenda kumtupa kwenye Pagala eneo ambalo siyo rahisi mtu kupita.

Kwa upande mwingine, DCP Msangi amesema upelelezi unaendelea wa kuwatafuta watu waliyohusika na mauaji ya mwanamke huyo kwa namna moja ama nyingine. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa ajili ya uchunguzi na utambuzi.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...