Skip to main content

Msafara wa Mkuu wa Wilaya Washambuliwa Kwa Mapanga Na Mishale

Msafara  wa Mkuu wa Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera, Godfrey Mheluka, umeshambuliwa na wananchi katika Kijiji cha Kashanda, Kata ya Nyakahanga alipokwenda kufuatilia mgogoro wa wafugaji na wakulima.

Katika mashambulizi hayo, Diwani wa Kata ya Nyakahanga, Charles Bechumila (CCM), amejeruhiwa vibaya kwa mishale na kukimbizwa katika Hospitali Teule ya Nyakahanga kutibiwa na alifanyiwa upasuaji huku hali yake ikielezwa kuwa ni mbaya.

Ilidaiwa kuwa mkuu huyo wa wilaya alikwenda kijijini hapo kutoa tamko kuhusu mgogoro wa wakulima na wafugaji akiwa na msafara wa magari mawili.

Katika gari lake alikuwa amepanda na Katibu Tawala wa Wilaya (DAS), Innocent Msena na Ofisa Uhamiaji mmoja na askari polisi wawili.

Gari la pili katika msafara huo lilikuwa na Diwani Bechumila, maofisa tarafa wawili na waandishi wa habari wawili wa Redio Karagwe.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustino Ulomi, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kubainisha kuwa askari waliokuwa wameambatana na mkuu wa wilaya walilazimika kufyatua risasi juu kutawanya washambuliaji, huku msafara huo ukikimbilia katika magari ambayo yalikuwa yameachwa umbali wa mita 600.

Ilielezwa kuwa Mkuu wa Wilaya alikwenda kuwaagiza wakulima kuhama eneo hilo kuwapisha wafugaji na tayari agizo kama hilo alikwishalitoa awali akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha Juni 5, mwaka huu.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...