Skip to main content

Makonda aomba msaada kwa jeshi la China kukabiliana na wauza dawa za kulevya


Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameomba msaada wa boti kwa jeshi la China kwa ajili ya kukabiliana na wahalifu wa madawa ya kulevya.

Makonda ameomba msaada huo alipotembelewa na viongozi  wa jeshi la China ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Makonda amewaomba kumsaidia kuwapatia vifaa vya kutumiwa  na askari wa doria katika Bahari ya Hindi   ili waweze kukabiliana na wahalifu wenye kuuza na kusafirisha madawa ya kulevya.
Pia Makonda ameeleza kuwa ujio wa viongozi  hao umejadili pia masuala mengi ya ushirikiano baina ya watu wa nchi hizi mbili na kuhakikisha usalama wa wao na ushirikiano mwingine wa nyanja mbalimbali.
Naye Mkuu wa Kikosi cha Maji  cha China (Navy),  Shen Hao, amepongeza juhudi za mkuu huyo wa mkoa  hasa za kuhakikisha anapambana na watu wanaoingiza madawa ya kulevya wakipitishia pembezoni mwa Bahari ya Hindi na akasema ushirikiano wa nchi yake  na nchi ya Tanzania utaendelea kuwa imara.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...