Skip to main content

Kituo Cha Afya Chalinze Chaanza Kufawanyia Oparesheni Wagonjwa

KITUO cha afya cha Chalinze kilichopo Kitongoji cha Bwilingu halmashauri ya Chalinze Bagamoyo Mkoa wa Pwani kimeanza kuwafanyia operesheni wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo kituoni hapo.

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mwanasheria Ridhiwani Kikwete ndiye aliyechokonoa hoja hiyo alipomtaka Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo kumpatia uhakika wa jambo hilo ambalo analisikia kwa watu kwamba Kituo hcho kimeshaanza zoezi la kuwafanyia upasuaji wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo.

"Nimesikia maneno kutoka kwa wakazi wakisema kwamba Kituo chetu cha afya Chalinze kimeshaanza kuwafanyia upasuaji wagonjwa wanaokwenda kwa ajili ya huduma hiyo, Mganga Mkuu tunaomba ulitaarifu Baraza hili taarifa hizo zilizo njema zina ukweli gani?," aliuliza Ridhiwani.

Akijibu swali hilo, Dr. Isaack Makungu aliwathibitishia Madiwani hao kwamba taarifa hizo zina ukweli na tayari akina mama 10 wajawazito wameshapatiwa huduma ya upasuaji kisha kupata watoto wakiwa salama na afya njema pamoja na wazazi wenyewe wakiwa na afya iliyo njema.

"Ni kweli Kituo chetu kimeshaanza kazi ya kuwafanyia upasuaji akina mama wajawazito ambao wamebainika hawana uwezo wa kusukuma mtoto ambapo watu kumi tumeshawapatia huduma hiyo wakiwa salama wao pamlja na watoto wao," alisema Dr. Makungu.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Said Zikatimu aliliambia Baraza hilo kwamba hatua hiyo ni faraja kwao kwani itasaidia mambo mengi kwanza kuwapunguzia saafari ndefu ya kwenda Tumbi, Bagamoyo au Muhimbili, poa mafuta ambayo yalikuwa yanatumika kusafirisha wagonjwa kweda maeneo nayo.

"Taarifa hiyo ni faraja kwetu kwani itasaidia wagonjwa ambao awali walikuwa wanasafirishwa kwenda Tumbi, Bagamoyo au Muhimbili, lakini tunatakiwa kujenga uzio kutoka chumba cha upasuaji kwenda wodini ili mgonjwa anapotoka kufanyiwa upauaji asiwe anaonekana na watu wengine," alisema Zikatimu.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...