Skip to main content

Kampuni ya mwana wa Abeid Karume yakumbwa na mlipuko Tanzania

Wakili Fatma Amani Abeid Karume ni mwana wa aliyekuwa rais wa Zanzibar Amani Abeid KarumeMakao makuu ya kampuni ya mawakili inayomilikiwa na wakili maarufu pamoja na mwana wa kike wa aliyekuwa rais wa Zanzibar Amani Abeid karume, Bi Fatma Karume mapema Jumamosi alfajiri yalikumbwa na mlipuko wa bomu.
Kampuni hiyo inaorodhesha kampuni za mawasiliano, kawi, benki pamoja na serikali kama mojawapo ya wateja wake.
Wakili Karume hivi karibuni amekuwa akimwakilisha kiranja wa upinzani bungeni Tundu Lissu mahakamani kwa mashtaka ya kuitusi serikali.
Bwana Lissu amekana mashtaka hayo.
Wakaazi wa eneo hilo katikati mwa mji wa Dar es Salaam wanasema walisikia misururu ya milipuko mikubwa muda wa saa nane alfajiri na muda mchache baadaye jumba hilo likajaa moshi na vifusi.
Mashahidi wengine wamesema kuwa walipata kifaa cha bomu la bomba.
Lakini maafisa wa polisi wamesema kuwa ni mapema mno kusema kuwa lilikuwa shambulio la bomu.
Mmoja ya mawakili wa kampuni hiyo amesema kuwa afisi yao iliharibiwa lakini hakuna kilichoibwa.
Rais wa chama cha mawakili wa Tanganyika Tundu Lissu ameshutumu shambulio hilo kama shambulio dhidi ya uhuru wa mawakili.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...