Skip to main content

Jinsi Ya Kutoka Katika Kifungo Cha Umaskini

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine kuna changamoto ambazo zinamkabili kuweza kupata mafanikio zaidi. Na hizo changamoto ndizo ambazo tunaziita kifungo cha umaskini, kwani kifungo hicho kinampelekea mtu huyohuyo kutokuwa na uhuru wa kipato, muda na kifikra.

Na kifungo hicho si kingine bali ni "uongo binafsi" hata hivyo tumia muda huu ili kusoma makala mwanzo mpaka mwisho haya utakwenda kujua kwa undani  maana ya kifungo hicho.

''If you want to success don't lie yourself'' ikiwa na maana ukitaka kufanikiwa usijidanganye mwenyewe. Msemo huu huwa naukumbuka sana kwani nilikutana nao katika pekuapekua zangu japo sikumbuki ni wapi hapo, ila naomba maana ipaki pale pale ili wabantu wenzangu na wasio wabantu waweze kuulewa msemo huo.

Niende moja moja kwa kujikita katika msemo huo, kwani msemo huo unayagusa maisha ya kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine matharani wewe unayesoma makala haya.

Mara kadhaa maisha yetu yamekuwa ni yale yale kwa asilimia kubwa hii ni kutokana na uongo ambao kila mmoja aweka ndani ya nafsi yake, na uongo huo huo bila kujali kama una madhara makubwa katika maisha yetu ndio tumekuwa tukiusujudu kwa namna moja ama nyingine.

Unajua binadamu huongozwa kwa asilimia kubwa na mtazamo, mtazamo huo huo umegawanyika katika makundi mawili hapa nina maanisha mtazamo chanya na mtazamo hasi.

Na pia kama unaamini katika kujifunza kama mimi utagundua ya kwamba watu wengi ambao wamefanikiwa, watu hao kwa kiwango kikubwa huwa na mtazamo chanya sana. Lakini ni kwanini watu wengi ambao hatupo katika mtazamo chanya maisha yetu daima yapo vilevile ?
Hii ni kutokana tumezoea kufanya vitu kawaida  kwa njia ile moja huku tukiamini mafanikio yanakuja kwakufanya hivyo. Kufanya hivyo ni kuendelea kujidanganya.

Wito wangu kwako kama nilivyoanza hapo juu tuache kujidanganya wenyewe kama kweli tunataka mafanikio . Huenda tangu hapo juu hadi nilipofikia hujanielewa mtu huwa anajidanganyaje? Shusha pumzi kidogo huku na mimi nikizidi kutumia halmashauri yangu ya kichwa na mamlaka ya mkono kukujuza zaidi kama ifuatavyo.

Binadamu ni kiumbe wa kujifajiri sana hata sehemu isiyo farijika unashangaa wala usishange afisa mipango nakandamiza kwa kupaka wino mweusi kwa kusema huo ndio ukweli.

Tujikite japo kwa sekunde chache japo ni nyingi kimaana katika kuuleza yafuatayo, tuangalie wafanyabiashara wangapi ambao hutumia vinywa vyao katika kuzidanganya nafsi zao ambazo huwa zinaathiri mafanikio yao kwa ujumla?
Ukijaribu kumuuliza mtu ambaye anafanya biashara kwamba biashara yake inaendeleaje? Hata kama biashara hiyo haiendi vizuri kiasi gani atakwambia biashara ni nzuri, mmh huku ndiko kujifariji kwenyewe, kwanini tusiwe wakweli wa nafsi zetu.

Hebu taangalie wale ambao ni wasomi ambao bado wanatumia kalamu zao katika kupata ujuzi zaidi, na hao hao ukiwauliza unaendeleaje na masomo hata kama anafeli kwa kiasi gani katika masomo yake utamsikia msomi huyo huyo atakwambia naendelea vizuri, aah tunakwenda wapi kwa kujifajiri kwa vitu ambavyo vimekuwa havitusaidii hata chembe zaidi kuendelea kufeli?
Siku zote tuache kujifariji kwa kuwadandanya wengine ya kwamba tunaendelea vizuri wakati uhalisia wake hauko hivo. Kuendelea kujidanganya wenyewe. binafsi ni sawa na kutumia muwa kama fimbo ya kutembea kwani utafika mahali utautafuna tu.

Inawezekana pia licha kuendelea kuidanganya nafsi yako kwa namna moja ama nyingine, umekuwa ukiitumia fimbo hiyo hiyo kuwafariji wengine na huku kufanya hivyo unahisi kutamsaidia mtu huyo kumbe ukweli na uhalisia wake haupo hivyo hata chembe.

Kuna usemi fulani ulikuja kwa ndege unaseme ''the only truth shall set you free" kwa kibantu ukiwa na maana "ukweli pekee ndio utaokuweka huru" haina haja ya  kuinua macho angani kutafakari katika kujua msemo huo maana unajieleza kabisa na upo wazi kwa maana unaeleweka kabisa.

Kuanzia sasa badili mtazamo wako kwa kuwa na fikra chanya ambayo itakufanya ujisemee ukweli, wewe binafsi na watu wengine kwani kufanya hivi kutakupa uhuru mkubwa kwa jambo ambalo unalifanya na huku matokeo ya kimafanikio yakija kwa upande wako kwa asilimia kubwa zaidi. Pia tuwakumbuke wahenga ambao wazidi kutupa hamasa kwa kusema hatma ya maisha yako unayo wewe mwenyewe.

Ni matumaini yangu makubwa unakwenda kubadilikia kuanzia sasa na mafanikio makubwa yatakwenda kuwa ukweli endapo utakwenda kuchukua hatua madhubuti zenye matokeo chanya.

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...