Skip to main content

Iraq yafanya mashambulizi ya ardhini kuuteka mji wa Tal Afar kutoka IS

Iraqi armoured vehicles are transported to the frontline outside Tal Afar (15 August 2017


Wanajeshi wa Iraq na makundi ya wapiganaji yanaounga serikali mkono wameanza mashambulizi ya ardhini katika mji wa Tal Afar, mojawepo wa ngome zilizosalia mikononi mwa kundi la kigaidi la Islamic state.

Mji huo umekuwa chini ya udhibiti wa Islamic state tangu mwaka 2014. Akihutubia taifa kupitia runinga,waziri mkuu Haider al-Abadi, amesema wapiganaji wa Islamic state huko Tal Afar wanafaa kujisalimisha ama wauwawe.

Shia paramilitary fighters take a rest during a live ammunition training exercise in Najaf city, southern Iraq, 14 August 2017Wapiganaji wa kiShia

Takriban wapiganaji 2000 wa Islamic state wanaaminika kuwa wamesalia katika mji huo, ambao umezingirwa tangu mwezi Juni, na umekuwa ukishambuliwa kutoka angani na ndege za kivita za Marekani na Iraq.
Raia Wengi walitoroka mji huo, japo 40,000 walibaki.
Ndege za jeshi la Iraq zimeshambulia ngome za IS katika mji huo kwa siku kadha, kuandaa mashambulizi ya ardhini
Map showing control of Iraq and Syria (14 August 2017)
Image captionIraq yafanya mashambulizi ya ardhini kuuteka mji wa Tal Afar kutoka IS

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...