Skip to main content

Gabriella aombwa kumaliza kesi ya Bi Mugabe nje ya mahakama

Bi Engels Gabriella aliyeshambuliwa na bi Grace MugabeBi Engels Gabriella aliyeshambuliwa na bi Grace Mugabe


Familia ya mwanamke aliyedaiwa kushambuliwa na bi Grace Mugabe imedaiwa kufuatwa na kuombwa na mtu asiyejulkani kukubali fedha kama fidia ya kutupilia mbali kesi hiyo , wakili wake amesema.
Familia haitaki kufanya hivyo, Gerrie Nel alisema.Walisema tuzungumze na tuwache kesi hii, lakini hakuna kiwango cha fedha kilichotajwa ,aliongezea.
Bwana Nel anajulikana kwa jina la utani kama ''the Pitbull''. Alifanikiwa kumshtaki mwanariadha mlemavu Oscar Pistorius kwa mauaji.
Wakati huohuo katika mahojiano marefu ya simu na bi Gabriella Engels ambaye amemtuhumu bi Grace Mugabe kwa kumpiga, Mwandishi wa BBC Pumza Fihlani alitulia na kuonekana kuwa mtu aliyekuwa na wasiwasi mwingi mara kwa mara.
Akielezea tukio hilo bi Engels mwenye umri wa miaka 20 alisema kuwa yeye na watu wengine wanne, wawili wakiwa wana wa kiume wa rais Mugabe na bi Grace Mugabe walikuwa wakinywa vinywaji siku ya Jumapili usiku katika chumba kimoja cha hoteli mjini Sandton, makaazi ya kifahari yaliopo Johannesburg.
Baadaye alienda katika chumba chengine na bi Mugabe akamfuata akiwatafuta wanawe.
Bi Mugabe alikuwa ameshikilia waya wa umeme mkononi mwake....alinizuia na kuanza kunipiga .
Nilijiangusha chini na kuanza kubingirika ili kukwepa kichapo hicho, na ni hapo aliponipiga na waya hiyo. Na nakumbuka nikiwa katika sakafu huku nikiwa nimejaa damu usoni na shingoni, bi Engels alidai.
Nilikuwa nikifikiria nitoke katika chumba hicho kabla ya mwanamke huyu kuniuwa.
Watu waliokuwa katika chumba hicho ni walinzi wake na walikuwa wamesimama nyuma yake huku akitupiga.
Tulimsihi kuwacha kufanya hivyo ,lakini hakutaka kusikia aliendelea kutupiga...alitupiga akiwa na chuki nyingi .
Sielewi kwa nini alitushambulia hivyo.

Bi Grace Mugabe

Comments

Popular posts

Ugonjwa wasababisha Manji kutofika mahakamani

Mfanyabiashara nchini, Yusuf Manji ameshindwa kufika mahakamani kusikiliza kesi yake inayomkabili kutokana na kuwa mgonjwa. Kesi hiyo ya uhujumu uchumi imeahirishwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutokana na mtuhumiwa huyo kutofika mahakamani hapo. Wakili wa serikali Estazia Wilson ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu, Godfrey Mwambapa kuwa Manji hajafika Mahakamani hapo kwa vile ni mgonjwa ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 25 mwaka huu itakapotajwa tena. Manji na watuhumiwa wenzake watatu wanakabiliwa na mashtaka saba yakiwemo ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya JWTZ, ukiwemo wa Mkuu wa Kikosi cha 21 JWTZ, wa Mkuu wa Kikosi Makutupora Dodoma (JWTZ) na wa Commanding Officer Korogwe na magari ya serikali. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Deogratius Kasinda na Thobias Pwere na mwingine ambaye jina lake halikufahamika mara moja, wote wamerudishwa rumande.

Mwanzo wa mwisho wa dunia utakuwa Jumatatu 21 Agosti?

Jua litapatwa na mwezi kikamilifu Amerika kaskazini kwa mara ya kwanza kabisa Jumatatu tangu 1918 Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani. Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani. Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana. Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa. Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia. Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa. Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri san...